Wednesday, 5 December 2018
Kilichotokea Sodoma na Gomora
Katika Biblia, imeelezwa
kuwa Sodoma na
Gomora iliangamizwa
na Mungu kwa sababu
wakazi wa miji hiyo
walizoelea maisha ya
dhambi. Kwa mujibu wa
kitabu cha Mwanzo 19:
24-25, “Ndipo BWANA
akanyesha juu ya Sodoma
na juu ya Gomora
kiberiti na moto toka
mbinguni kwa BWANA.
Akaangusha miji hiyo
na Bonde lote, na wote
waliokaa katika miji
hiyo, na yote yaliyomea
katika nchi ile.”
Utafiti wa wanasayansi
ambao matokeo yake
yamewekwa wazi hivi
karibuni, umethibitisha
kile ambacho wasomi
wa Biblia walikijua
siku nyingi, kwamba
maangamizi kutoka
mbinguni yaliharibu
mfumo wote wa maisha
katika eneo la Bahari
Mfu [Dead Sea] miaka
maelfu kadhaa iliyopita.
Baada ya kutumia
karne nzima
wakifanya uchunguzi,
mwanaaikolojia Profesa
Philip Salvian wa Chuo
Kikuu cha Trinity
Southwest kilichopo
Albuquerque, New
Mexico, Marekani,
amezungumzia utafiti
wake na wenzake,
katika mkutano wa
mwaka wa watafiti wa
Kimarekani wa masuala
ya Mashariki ya MbaliAmerican
Schools of
Oriental Research, hivi
karibuni
Wanasayansi hao
wanaamini kuwa
wamegundua maeneo
ya miji hiyo kupitia
uchunguzi wa
kiaikolojia, lakini
wametoa maelezo zaidi
ya kisanyansi kwamba
kwanini maeneo hayo
yaliteketezwa kabisa.
W a n a i k o l o j i a
wanaeleza kuwa miji
ile ilikuwa kaskazini
mashariki ya Bahari Mfu
[Dead Sea], ambako sasa
panaitwa Middle Ghor.
Kinachofurahisha ni
kwamba katika maeneo
hayo, wanasayansi
wamegundua madini ya
ajabu ambayo wanasema
yanatokana na jiwe
lililopasuka kutokana
na joto kali katika
ukanda huo.
Mbinu za rediokaboni
[ r a d i o c a r b o n ]
zinaonyesha kuwa
mlipuko huo wa jiwe
ulitokea miaka kama
3,700 iliyopita-ambayo
inaweza kuendana
na muda wa kibiblia
unaohusishwa na tukio
hilo.
Watafiti hao wameuita
mlipuko huo wa jiwe
kuwa ni 3.7KYrBP
Kikkar na ulikuwa na
kipimo cha megatani 10.
[Megatani 1 ni sawa na
kilotani 1000].
Muiakolojia huyo wa
chuo kikuu cha Trinity
Southwest ambaye pia
ni mtafiti wa Biblia,
Phillip Silvia anasema
mlipuko huo unaweza
kuathiri eneo lenye
ukubwa wa kilometa 25,
na kuangamiza makazi
yoyote yaliyo karibu.
Profesa Silvia anasema
kuwa yeye na timu yake
wamekuwa wakiufanyia
utafiti mji wa Zama
za Shaba wa Tall elHammam,
karibu na
Sodoma na Gomora,
na ni eneo hilo ambalo
linatoa ushahidi
mkubwa wa mlipuko
huo.
Profesa Silvia na timu
yake wameandika katika
tovuti yao ya mradi
wa utafiti katika eneo
hilo-Tall el-Hammam
Excavation Project: “Mji
huo [unaweza kuwa]
ulianza katika milenia
ya 4 KK, na kustawi kwa
miaka elfu moja kama
eneo la wazi la jamii ya
wakulima.
“Lakini mwanzoni
mwa milenia ya 3
KK, jambo la ghaf la
kuhusiana na amani ya
eneo hilo lililotokea,
na kusababisha watu
wa Tall el-Hammam
kujenga mfumo wa
kujilinda uliohusisha
kujizungushia ukuta wa
mawe na tofali za tope”.
Silvia ameongoza
utafiti katika maeneo
makubwa matano ya
Yordani pembezoni
mwa Mto Yordani. Kwa
mujibu wa Profesa Silvia,
eneo lenye ukubwa wa
maili za mraba 15 za
Middle Ghor lilikuwa
bonde lenye rutuba,
likiendelea kukaliwa na
watu kwa miaka kama
2,500 hivi. Maangamizi
yaliyotokea miaka 3,700
iliyopita yalisababisha
mwisho wa ghaf la wa mji
huo, na kuteketeza watu
wote wanaokadiriwa
kuwa kati ya 40,000
hadi 65,000 walioishi
katika eneo hilo wakati
huo.
Tukio hilo la
maangamizi lilikuwa
kubwa kiasi kwamba
eneo hilo lilibaki bila
kukaliwa na watu kwa
miaka 600.
Wasomaji wa Biblia
wanafahamu kuwa miji
ya Sodoma na Gomora
iliteketezwa kwa
moto baada ya Mungu
kuihukumu kwa sababu
ya uasherati uliokuwa
ukifanyika ndani yake.
Mwanzo 19:4-25.
Katika kitabu cha Yuda
1:7 Biblia inasema: “Kama
vile Sodoma na Gomora,
na miji iliyokuwa kandokando,
waliofuata
uasherati kwa jinsi moja
na hawa, wakaenda
kufuata mambo ya
mwili yasiyo ya asili,
imewekwa kuwa dalili,
wakiadhibiwa katika
moto wa milele.””
Ikiwa Mungu aliwatenda
hivi watu wa Sodoma
na Gomora, ni kitu gani
kinamfanya mwanadamu
wa leo afikiri kuwa
Mungu amebadilika juu
ya kuadhibu wale wote
wafanyao uasherati?
Katika miji hiyo miwili
ni watu watatu tu
waliobaki ambao ni Lutu
na watoto wake wawili.
Wanadamu wengine
wote waliokuwa katika
miji hiyo waliteketezwa
kwa sababu ya zinaa.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
-
SOMO: TAMBUA MAJIRA NA NYAKATI Luka 19:41-46 41 Alipofika karibu aliuona mji, akaulilia, 42 akisema, Laiti ungalijua, hata wewe katika...
-
SHETANI ANAWEZA KUTUMIA KAZI YA MTU KUMLETEA MTU HUYO UHARIBIFU. Bwana YESU atukuzwe ndugu yangu. Karibu tujifunze Neno la MUNGU. L...
-
Katika Biblia, imeelezwa kuwa Sodoma na Gomora iliangamizwa na Mungu kwa sababu wakazi wa miji hiyo walizoelea maisha ya dhambi. Kwa mujib...
No comments:
Post a Comment