Friday, 7 December 2018

ROHO MTAKATIFU ANAVYOONGOZA WANA WA MUNGU KUTEMBEA NA MUNGU KATIKA MAENEO MBALIMBALI YA MAISHA YAO (SEHEMU YA 1)

Jina la Yesu Kristo litukuzwe milele!

Leo nataka kuanza mfululizo mwingine wa somo, ambao naamini utakuwa wa msaada sana kwako, katika kuimarisha uhusiano wako na Mungu.
Somo lenyewe ni hili: “ROHO MTAKATIFU ANAVYOONGOZA WANA WA MUNGU KUTEMBEA NA MUNGU KATIKA MAENEO MBALIMBALI YA MAISHA YAO”.
Mfano na 1: Tunaposoma kitabu cha Matendo ya Mitume 27:10, tunaona jinsi mtume Paulo alivyoarifiwa na Roho Mtakatifu, juu ya hatari iliyokuwa mbele yake, katika safari aliyokuwa nayo na wenzake.

Mtume Paulo akawaambia wenzake hivi: “naona kwamba safari hii itakuwa na madhara na hasara nyingi si ya shehena na marikebu tu, ila na ya maisha yetu pia”. Na jambo hili likatokea kweli kama alivyosema!
Swali la msingi la kujiuliza hapa ni kutaka kujua mtume Paulo alijuaje juu ya hatari ile! Roho Mtakatifu alitumia njia gani kumjulisha kwa uwazi namna ile? Je, na sisi leo Roho Mtakatifu anaweza kutujulisha juu ya hatari zilizo mbele yetu na tukauelewa ujumbe wake?

Mfano na 2: Je! Unafahamu mtume Paulo na wenzake walikuwa wanaamuaje juu ya eneo la kwenda kupeleka neno la Mungu? Ukisoma habari zao kwenye biblia, utajua ya kuwa ni kwa msaada wa uongozi wa Roho Mtakatifu.
Kuna wakati walikuwa wakipita nchi za Frigia na Galatia zilizokuwa Asia, wakitaka kulihubiri neno la Mungu huko. Biblia inasema walikatazwa “na Roho Mtakatifu, wasilihubiri lile neno katika Asia” (Matendo ya Mitume 16:6).
Biblia inaendelea kutueleza juu ya safari yao hiyo ya kwamba: “Walipofika kukabili Misia wakajaribu kwenda Bithinia, lakini Roho wa Yesu hakuwapa ruhusa” (Matendo ya Mitume 16:7). Na baada ya hapo, Roho akawapa kufahamu kuwa, walitakiwa kwenda Makedonia kuhubiri neno huko. Na ndivyo walivyofanya!

Swali la msingi la kujiuliza hapa, ni kutaka kujua walijuaje kuwa katika wazo walilokuwa nalo, Roho Mtakatifu alikuwa anawakataza wasilifanye, au anawanyima ruhusa wasilifanye? Na ikiwa Roho Mtakatifu ana wazo analotaka walitekeleze walilijuaje?
Je! Kwetu sisi – tulio wana wa Mungu kipindi hiki, tunaweza kupata msaada wa Roho Mtakatifu kuhusu mahali pa kwenda, au mahali pa kutokwenda, kama akina mtume Paulo walivyosaidiwa?
Na ikiwa ni hivyo – ina maana si suala la mtoto wa Mungu kuamua kwenda mahali popote atakavyo, bali hili ni muhimu ajue wazo la Roho Mtakatifu aliye naye ndani yake kuhusu safari yake hiyo!

Mfano na. 3: Roho Mtakatifu ndiye aliyemsaidia Yesu kuchagua wanafunzi wake kumi na wawili. Biblia inasema habari hizi za Yesu ya kuwa: “Ikawa siku zile aliondoka akaenda mlimani ili kuomba, akakesha usiku kucha katika kumwomba Mungu. Hata kulipokuwa mchana aliwaita wanafunzi wake; akachagua kumi na wawili miongoni mwao, ambao aliwaita Mitume” (Luka 6:12,13).
Habari hii haituambii moja kwa moja ni kwa namna gani, na kwa njia gani Yesu aliweza kufanya maamuzi ya nani amchague, na nani asimchague “miongoni” mwa wanafunzi wengi aliokuwa nao wakati ule!

Kwa msomaji yeyote wa biblia, anajua ni Roho Mtakatifu aliyemsaidia kufanya uchaguzi wa watu wa kukaa naye karibu! Lakini swali la kujiuliza ni kutaka kujua Roho Mtakatifu alimsaidia kwa njia zipi?
Nina uhakika tukijua jinsi Yesu alivyosaidiwa katika hili, itakuwa ni rahisi kwetu kusaidiwa na Roho Mtakatifu kujua watu wa kuwa nao karibu, na watu wa kukaa nao mbali! Pia naamini tunaweza kujua ni nani wa kushirikiana naye, na ni nani wa kutoshirikiana naye!

Biblia inasema katika Warumi 8:24 tunasoma ya kwamba: “wote wanaoongozwa na Roho wa Mungu, hao ndio wana wa Mungu”.
Na Yesu akizungumza juu ya Roho Mtakatifu atakapokuja kwenye maisha ya wanafunzi wake alisema: “Lakini yeye atakapokuja huyo Roho wa kweli, atawaongoza awatie kwenye kweli yote;…na mambo yajayo atawapasha habari yake” (Yohana 16:13).
Nataka ujue ya kuwa, ikiwa wewe ni mtoto au mwana wa Mungu, ni haki yako itokayo kwa Baba yako, yaani Mungu, kuongozwa na kutegemea kuongozwa na Roho Mtakatifu!

Uwe mtumishi wa Mungu au usiwe mtumishi wa Mungu – ili mradi tu wewe ni mtoto wa Mungu; Roho Mtakatifu uliye naye amepewa jukumu la kukusaidia, ikiwa ni pamoja na jukumu la kukuongoza katika maisha yako ya kila siku!
Ndani ya mfululizo wa somo hili, tutajifunza njia kadhaa anazotumia Roho Mtakatifu kumwongoza mwana wa Mungu.

1 comment:

  1. Ushuhuda Wangu wa Kutoka Moyoni 💖

    Baada ya baba yangu mdogo kuniacha kwa miezi saba mirefu, nilikuwa nimevunjika moyo kabisa. Alinizuia kwenye mitandao yote ya kijamii, akaondoka, na hakukuwa na njia ya kumfikia. Karibu nikate tamaa, lakini ndani kabisa nilijua singeweza kupata mtu yeyote ambaye angenipenda na kunitendea jinsi alivyonitendea.

    Siku moja, bosi wangu kazini aligundua jinsi nilivyokuwa na huzuni na akanitambulisha kwa Dkt. Dawn. Dkt. Dawn alisikiliza hadithi yangu na akaahidi kwamba mpenzi wangu angerudi kwangu ndani ya siku tatu. Kwa kweli, sikuamini mwanzoni—lakini kwa mshangao wangu mkubwa, siku ya tatu simu yangu iliita. Ilikuwa yeye! Alikuwa akilia na kuomba msamaha, akisema hataniacha tena.

    Tangu siku hiyo, uhusiano wetu umekuwa na nguvu na uzuri zaidi kuliko hapo awali. Amekuwa akipenda na kunijali mimi na mtoto wetu, na sasa tunafunga ndoa katika miezi miwili tu! ❤️

    Shukrani zote kwa Dkt. Dawn, ambaye kwa kweli alifanya jambo lisilowezekana liwezekane. Ninampendekeza kwa moyo wote kwa yeyote anayekabiliwa na changamoto katika:

    Masuala ya uhusiano au ndoa

    Ugonjwa au magonjwa

    Matatizo ya utasa au bahati nasibu

    Kesi za mahakamani au urejeshaji wa mali

    Dkt. Dawn kweli hutatua matatizo kwa ufanisi na hurudisha furaha katika maisha ya watu.

    Wasiliana na Dr. Dawn kwenye WhatsApp: +2349046229159
    Barua pepe: dawnacuna314@gmail.com

    ReplyDelete